Na Clarence Chilumba, Nachingwea
WANANCHI wilayani hapa mkoani Lindi, wameombwa kuchagua viongozi
makini na wenye sifa ya kuliongoza taifa.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), mkoa wa Lindi, Amiri
Mkalipa, alitoa ombi hilo jana, wakati wa uzinduzi wa kampeni za CCM
zilizofanyika katika viwanja vya Mauridi mjini hapa.
Alisema wananchi wanapaswa kuwa makini kipindi hiki ili kuchagua
viongozi wenye sifa ambao wanatoka CCM.
Alisema kwa kipindi cha miaka kumi ya uongozi wa Rais Jakaya
Kikwete, ameweza kuboresha huduma za kijamii, ikiwemo miundombinu ya barabara,
elimu, afya, kilimo na maji.
Kwa upande wake, mgombea ubunge wa jimbo la Nachingwea, Hasani
Masala, alisema kilichomsukuma kuwania nafasi hiyo ni kuwatumikia wananchi wa
wilaya hiyo.
Aliwaomba wananchi wamchague ili aendele kuboresha huduma
mbalimbali za kijamii, ikiwemo maji safi na salama, elimu na afya.
Masala alisema katika kipindi cha uongozi wake, atahakikisha
anaisimamia halmashauri ya wilaya hiyo ili iweze kuongeza mapato na kunyanyua
uchumi wa wananchi.
Aidha, alisema atahakikisha kilimo kinaboreshwa kwa kuongeza zana
za kisasa, ikiwemo matrekta na kwamba atasimamia kwa ukaribu kuona
wakulima wananufaika na mfumo wa ununuzi wa mazao.
No comments:
Post a Comment