Friday, 18 December 2015

CHINA YATOA VITANDA 60 KWA HOSPITALI YA LINDI

 Balozi wa China nchini Dk. Lu Youqing akizungumza kabla ya kukabidhi vitanda 60 vya kujifungulia wakina mama katika mkoa wa Lindi, kushoto ni mkalimani wake Ndugu Mu Lin.
Nape na Balozi Lu wakiangalia vitanda hivyo
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (MB) akizungumza kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (MB) ambapo alisema Serikali ya China pamoja na watu wake wamekuwa marafiki wa kweli kwa Tanzania na wamekuwa wakitoa misaada mingi bila kutoa masharti.
 Balozi wa China nchini Dk. Lu Youqing pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mtama wakiwasili katika kata ya Kiwalala, jimbo la Mtama tayari kwa kukabidhi vifaa vya matibabu katika Zahanati ya Mauhumbika.

No comments:

Post a Comment