Saturday 10 October 2015

DK SHEIN ANAZO SIFA KULIKO WOTE




JUMUIA ya Wazazi CCM imemtaja mgombea wa Urais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein ni mtu mwenye uwezo mkubwa kuliko viongozi wote wanaogombea nafasi hiyo visiwani hapa.
Pia imesema ahadi anazotoa mgombea wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad kuwa akichukua urais ataibadilisha Zanzibar na kuwa Singapore ni uongo mkubwa.
Naibu Katibu Mkuu wa Wazazi Zanzibar, Najma Giga, alisema Maalim Seif si mtu makini na anachokizungumza hakijui  ndiyo maana amekuwa mtu wa kusema kila kitu.
Alisema Maalim Seif ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, na ni mtu muhimu kwa Rais Dk. Shein kwa sababu ana uwezo wa kumfuata au kumpigia simu muda wowote kama ana njia za kuifanya Zanzibar kuwa Singapore.
"Sasa kama ameshindwa kumshauri Dk. Shein ili aifanye Zanzibar kuwa Singapore ndani ya miaka mitano atawezaje kuifanya kwa siku 100. Wazanzibari tusidanganywe na huyu mtu ni mwongo sana,” alisema.
Alisema Dk. Shein ameweza kufanya mambo mengi ikiwemo kuhakikisha kuwepo kwa amani ya kudumu na hata kukifanya Chama Cha Mapinduziv (CCM) kutembea kifua mbele kutokana na kutekeleza mambo mengi.
Alisema mtu sahihi wa kuipa Zanzibar maendeleo ni Dk. Shein kwa kuwa ni mmoja wa kiongozi bora na mwenye maono ya mbali katika kuipa sifa Zanzibar.
Katika hatua nyingine, Naibu Katibu Mkuu huyo aliwataka waangalizi wa kimataifa wa uchaguzi waliokuja visiwani hapa.
Alisema litakuwa jambo la ajabu, endapo waangalizi hao watashindwa kufuata taratibu zilizowekwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) na badala yake kutenda mambo kinyume na wanavyotakiwa.
Kwa mujibu wa Naibu Katibu Mkuu huyo, endapo waangalizi hao watashindwa kufuata taratibu hizo, watashindwa kuandika ripoti zitakazotokana na uchaguzi huo.
@@@
Watakiwa kupewa elimu ya mpigakura
WAZANZIBAR wametakiwa kupewa elimu ya mpigakura na Tume ya  Uchaguzi Zanzibar (ZEC) katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.
Pia wananchi walioshindwa kuchukua shahada zao za kupigia kura wanapaswa kwenda ofisi za ZEC kuchukua vitambulisho hivyo ili waweze kupiga kura.
Naibu Katibu Mkuu wa Wazazi, Najma Giga, alisema wananchi wa Pemba na Unguja wanapaswa kushiriki kwa wingi kwenye uchaguzi huo, kwa kuwa ni haki yao kikatiba.
Alisema tunaiomba ZEC itoe elimu kwa mpigakura lakini pia sisi jumuia tunawaomba wananchi kuwa katika karatasi ya mpigakura wakiona picha ya Dk. Ali Mohamed Shein, waweke alama ya vema.
Naibu Katibu Mkuu huyo, alisema kila mwananchi anapaswa kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura ifikapo Oktoba 25, mwaka huu kwa kuwa ndiyo fursa muhimu ya kuhakikisha Dk. Shein anaendelea kubakia madarakani.

No comments:

Post a Comment