Wednesday 7 October 2015

ASKOFU AWATAKA WATANZANIA KULINDA AMANI




Na Clarence Chilumba, Masasi
ASKOFU wa Kanisa la Sayuni International Pentekoste, Masasi mkoani Mtwara, Angelus Mchomanjoma, amewataka Watanzania kuilinda amani iliyopo ambayo ni tunu kwa taifa.

Alitoa wito huo jana wakati akizungumza na Uhuru kuhusu maandalizi ya tamasha la kuombea amani mkoa wa Mtwara, litakalofanyika keshokutwa kwenye viwanja vya Boma mjini Masasi.

Alisema lengo la tamasha hilo ni kuombea amani ili matokeo ya uvunjifu wa amani yasijitokeze kipindi hiki cha kampeni na baada ya matokeo kutangazwa na kwamba rais atakayechaguliwa ndiye chaguo la Mungu.

Mchomanjoma alisema tamasha hilo la kuombea amani mkoani Mtwara litashirikisha maaskofu,wachungaji pamoja na waimbaji kutoka kwenye kwaya mbalimbali za makanisa ya Kipentekoste kutoka ndani na nje ya mkoa huo.

Alisema tamasha hilo lenye lenye kauli mbiu ya ‘Umoja wetu ndio msingi wa amani yetu’, ni sehemu muafaka kwa maaskofu na wachungaji wa umoja wa makanisa hayo, kuhubiri neno la Mungu kwa ajili ya kulinda na kuitetea amani kipindi chote cha uchaguzi.

No comments:

Post a Comment