Monday 12 June 2017

KAULI ZA UCHUNGU ZILIZOTOLEWA NA RAIS MAGUFULI BAADA YA RIPOTI HIYO KUTOLEWA



Rais Dkt. Magufuli alianza kwa kusema "Mtanzania yoyote mwenye akili timamu ukisikia ripoti kama hii inatia uchungu sana, na ndio maana nashindwa hata niazie wapi"

"Mwenyezi Mungu alituwekea rasilimali nyingi ili zitunufaishe Watanzania...madini tuliyonayo Watanzania ni madini ya kila aina na wala sio machache"

"Kampuni inafanya biashara ya trilions of money lakini hata haijasajiliwa nchini!! Mara ngapi tunawaumiza wamachinga wasio na leseni?".

"Wanasheria wapo tu, eti wanaogopa kushtakiwa. Yani mali yangu, mimi ndio nakulindia biashara yako, halafu uniibie, ukanishtaki, bado nikuache uchimbe?"

"Pamoja na mali hii yote, Mungu kutupendelea watanzania tumeendelea kuwa masikini, nina uhakika hata shetani aliko kule anatucheka kwa umasikini wetu ni wa kujitakia, lakini shetani huyu huyu tunayemlani inawezekana aliwatumia baadhi ya Watanzania wakati wakiwa ni viongozi"

"Wapo watanzania wenzetu waliopewa madaraka na Watanzania masikini kwa ajili ya kusimamia rasilimali zetu, lakini wamekuwa part ya kuwaibia Watanzania masikini"

"Kuna kampuni 6 ambazo wao hununua makinikia bila hata kuyaangalia kwa sababu wanajua kuna mali ndani."

"Mawaziri na wasaidizi wao kila siku wanaenda Ulaya lakini hawataki hata kukosea njia kwenda kuona hizo smelters".


No comments:

Post a Comment