NA SELINA WILSON,
KILOSA
MGOMBEA
urais wa CCM, Dk. John Magufuli maarufu Tingatinga, amebomoa ngome ya CHADEMA
wilayani Kilosa mkoani Morogoro kwa kumchukua Mwenyekiti wa Wilaya wa chama
hicho, Selemani Simba.
Dk.
Magufuli alimpokea mwenyekiti huyo pamoja na timu ya wananchama wa CHADEMA
zaidi ya 50 akiwemo Katibu Mwenezi wa Kilosa Kati, Mussa Ngongi.
Akizungumza
kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mjini Kilosa, Simba alisema ameamua
kujitoa CHADEMA, baada ya kuchoshwa na siasa za upinzani.
“Nimeamua
kutoka CHADEMA baada ya kuona amepatikana mzalendo wa kweli Dk. Magufuli ambaye
anatosha kuwa Rais wa Tanzania. CHADEMA hawana uzalendo wamesimamisha fisadi
kuwa mgombea urais,” alisema.
Kwa
upande wake Musa Ngongi aliyekuwa Katibu wa Jimbo la Kilosa wa CHADEMA, alisema
amejiunga na CCM ili akafanye siasa safi na za kizalendo.
“Nitapinga
nini wakati Dk. Magufuli ni mzalendo na ndio mgombea wa CCM, sioni sababu
ya kuendelea kuwa mpinzani sioni cha kupinga,” alisema.
Alisema CHADEMA
wameungana na Lowassa ambaye wakati wa safari za matumaini, Mwenyekiti wa
CHADEMA, Freeman Mbowe, aliwahi kusema kwamba anashangaa majambazi wanachomwa
moto lakini Lowassa anachwa anatamba wakati yeye ni miongoni mwa mafisadi papa.
Ngongi
alisema alisema kutokana na kitendo hicho amepoteza ujasiri wa kuendelea kubaki
ndani ya CHADEMA hivyo, ameamua kujiunga na CCM kwa ajili ya kumpigania Dk.
Magufuli na madiwani na wabunge wake.
Kwa
upande wake aliyekuwa mpambanaji wa CHADEMA, Oliva Mollel, alisema amemua
kuhama kwa kuwa hakuna matumaini kwenye chama hicho.
“Nilikuwa
CHADEMA kiherehere. Tulikuwa tunapiga vita ufisadi lakini sasa kumekuwa na
ufisadi ndani ya CHADEMA, nimeamua kutoka na sasa na naomba vijana wenzangu
tupambane na ufisadi kwa nguvu zote tumchague Dk. Magufuli,” alisema.
Dk.
Magufuli alifanya mikutano ya kampeni katika maenei ya Kimamba,Melela na
Sanganga njia pande ya kwenda Mzumbe, ambapo aliwataka wananchi
kuichagua CCM ili ifanye kazi ya kudhibiti mafisadi.
Alisema
atahakikisha sekta za elimu, afya, maji, barabara zinaboreshwa kwa ajili ya
maendeleo ya wananchi.
No comments:
Post a Comment