Monday 7 December 2015

TANESCO YAWATIMUA KAZI MAOFISA WAKE WANANE


Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
SHIRIKA la Umeme nchini (Tanesco) limewafukuzisha kazi watumishi waandamizi wa Tanesco upande wa maneja na wahasibu kutokana na ubadhirifu wa fedha katika utumishi wao.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Felschimi Mramba amesema kuwa shirika halitaweza kuwaacha watendaji wakawa wanafanya kazi kwa rushwa wakati wanalipwa mishahara.
Amesema wataendelea kuchukua hatua kwa watendaji wote watakabainika kufanya udanganyifu au kutoa lugha zisifaa kwa wateja na wakati mwingine kuomba fedha kwa huduma ambazo ni haki ya mwananchi kupata.
Mramba amesema Tanesco imeongeza uzalishaji wa umeme unaotumia gesi megawati 300  sawa na asilimia 115  na kufanya kuwa na umeme wa uhakika huku miradi mingi ikiendelea kufanyika.
Amesema  wanatarajia kupata megawati 240 kutoka Kinyerezi namba mbili  wakati wowote  na kufanya shirika kuwa na umeme wa uhakika.
Aidha amesema wakati wa suala miundombinu likifanyiwa kazi wananchi wawe wavumilivu wa kukatika umeme katokana na kuboresha miundombinu hiyo.
Aliongeza kuwa wanaotaka kufanya kazi na Tanesco kwa kupata nguzo lazima wazalishe nguzo zenye ubora wa kuweza kuhimili kwa muda mrefu bila kuanguka kuanguka.

No comments:

Post a Comment