Tuesday 5 January 2016

MHANDISI LWAKATARE KUIONGOZA DART




MHANDISI Ronald Lwakatare ameteuliwa  kuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka  Jijini Dar-es- Salaam (DART).

Uteuzi huo umefanywa  juzi na Waziri  wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene.

Akisoma taarifa hiyo kwa niaba ya Simbachawene, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini , Ofisi ya Rais TAMISEMI, Rebecca Kwandu, alisema  uteuzi huo ulianza juzi.

Rebecca alisema Simbachawene amefanya uteuzi huo kutokana na mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 2 (2) cha amri ya kuanzisha wakala huo wa DART, tangazo la serikali namba 120 la mwaka 2007.

Alisema uteuzi huo unafuatia kusimishwa  kazi kwa aliyekuwa Mtendaji Mkuu, Asteria Mlambo, aliyesimamishwa Desemba 23, mwaka jana.

Asteria alisimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi dhidi yake  kutokana na tuhuma mbalimbali zinazomkabili kuhusiana na wakala huo.

Rebecca alisema awali, Mhadisi Ronald alikuwa Naibu Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Mfuko wa Barabara, akishughulikia  ufuatiliaji na tathmini.

Alisema mtendaji huo mpya anatakiwa kuripoti kazini na kuanza kazi mara moja.

No comments:

Post a Comment