BLANDINA
ARISTIDES, MWANZA
MWENYEKITI
wa CCM mkoani hapa, Antony Dialo, amewataka wanachama wa CHADEMA kuomba gawio
la fedha kutoka kwa viongozi wao waliokiuza chama hicho kwa Waziri Mkuu
aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, Edward Lowassa, ili nao wafaidike.
Alisema
hayo jana, wakati akizindua kampeni za chama wilayani Ilemela, ambapo alidai
kuwa chama hicho kwa sasa si mali ya wanachama bali ni mali ya Lowassa na washirika wake ambao ni makapi yaliyotemwa
na CCM.
“Kuna
watu watatu ambao ni wajanja kwenye siasa hao ni Mtei (Edwin), Mbowe (Freeman)
na Ndesamburo (Phillimon), hawa ni wafanyabiashara na tayari wamemaliza hiki
chama, hivyo wanachama wawaombe gawio la fedha ili nao wafaidi,” alisema Dialo
na kushangiliwa na umati wa wananchi uliojitokeza.
“Tunapokwenda
kanisani tuwaombe CHADEMA ili ujinga uwatoke, maana hata wakiambiwa hawaelewi, wanabaki
kung’ang’ana na kupambana na CCM, eti waitoe madarakani na ukiwauliza sababu ya
kuwaondoa CCM hawana jibu, wanasema lazima tuiondoe tu jambo ambalo
haliwezekani” alisema.
Naye
Katibu wa CCMma Mkoa wa Mwanza, Miraji Mtaturu, alisema alitegemea upinzani
ndio ujenge misingi ya kuleta maendeleo lakini umegeuka kuwa vyama vya usanii
na ndio maana upinzani walikosa mgombea urais.
Mtaturu
alisema kutokana na sababu hiyo,
waliamua kumchukua mgombea kutoka CCM, ambaye hivi sasa anawatesa.
“CHADEMA ni sawa na kupe ambaye aking’ang’ania
kwenye ng’ombe hatoki hata kama ng’ombe atachinjwa yupo tu, watu wamekalia
peoples …! wakati chama kilishauzwa na pesa ilishaliwa kitambo,” alisema
Mtaturu.
Mgombea
ubunge wa Jimbo la Ilemela, Anjelina Mabula, alisema atahakikisha Ilani ya
Uchaguzi ya CCM anaisimamia na kuitekeleza kwa asilimia 100.
Alivitaja
vipaumbele vyake kuwa ni afya ya mama na mtoto, elimu na miundombinu.
Mwalusamba:
Hata waovu
wanafanya
uamuzi mgumu
NA SHAABAN MDOE, ARUSHA
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC)
ya CCM, Godfrey Mwalusamba, amewataka wakazi wa Jiji la Arusha, kupingana na
kauli ya uamuzi mgumu wa kuikataa CCM.
Alisema mfano unaotolewa na wapinzi
haustahili kufuatwa, kwani utawapotosha.
Aidha, amesema hakuna mgombea urais
mwenye sifa kama Dk. John Magufuli, kutokana na uadilifu na uchapakazi alionao na
aliouonyesha katika miaka ishirini aliyokaa serikalini.
Mwalusamba aliyasema hayo alipokuwa
akizungumza katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za mgombea ubunge na madiwani
wa Jimbo la Arusha ulioongozwa Dk. Mary Nagu.
Alisema wapo watu ambao wanaweza kukubalika pindi wanaposema watachukua uamuzi mgumu, hata kwa kuwaangalia usoni, akiwemo Dk. Magufuli, lakini siyo Lowassa, ambaye tayari ana makandokando mengi, ikiwemo kashfa ya Richmond iliyomfanya ajiuzulu nafasi ya uwaziri mkuu.
Aliongeza kuwa mbali na kashfa hiyo
ya Richmond pia mgombea huyo anatia shaka kutokana na kuchangiwa fedha na
wafanyabiashara, jambo ambalo limekuwa likihojiwa atalipa fadhila gani iwapo
atashinda.
Mwalusamba aliwataka wananchi kukaa
na kutafakari na kisha kumwuuliza atawadhibiti vipi matajiri hao pindi
watakapofanya ufisadi kwa ujasiri kutokana na michango yao kwake katika safari
yake hiyo.
Alisema Dk. Magufuli hana deni na
mtu yoyote aliyemchangia katika safari yake ya urais na kwamba mgombea wa CCM
yupo na watu masikini, walio na mategemeo makubwa toka kwake.
Aliwataka wakazi wa Jimbo la Arusha
kumchagua mgombea wa ubunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Philemon Mollel
pamoja na madiwani wake, kwakuwa mgombea huyo ana uwezo wa kuwatumikia
wananchi.
Dk. Mary aliwataka wananchi
kutokubali kudanganywa tena na kumchagua mbunge wa upinzani, ambaye hajawasaidia
lolote, zaidi ya yeye na familia yake.
Kwa upande wake, Mollel alisema
iwapo atachaguliwa atahakikisha anajenga masoko yote, ambayo yatakuwa ya
ghorofa ili wafanyabiashara wote wapate maeneo.
Alisema atahakikisha vikundi vya
akina mama anavikopesha zana za kilimo na biashara alizonazo, ili ziwawezeshe
kujikwamua kiuchumi.
Mabula azidi kutisha,
Wenje maji ya shingo
NA PETER KATULANDA, MWANZA
ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la
Nyamagana, Ezekia Wenje (CHADEMA), juzi aliandamana na wafuasi wake ,kitendo
ambacho kimetafsiriwa kuwa alikuwa akiwaaga rasmi wananchi wa jimbo hilo,
kutokana na mambo kuonekana kumeendea kombo.
Wenje aliandamana kabla ya kuzindua
kampeni kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mbugani, baada ya kuahirisha uzinduzi
huo mara tatu, akihofia kukosa watu kama
waliohudhuria mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM, zilizofanyika kwenye
uwanja huo, mwishoni mwa mwezi uliopita.
Kama kawaida ya CHADEMA kukodi na
kusomba watu kutoka wilaya na mikoa jirani, mkutano huo pia ulijaa watu kutoka
nje ya Mwanza na kuhudhuriwa na vigogo wanane wa chama hicho.
Hata hivyo, wakati Wenje akizindua
kampeni zake katika Kata ya Mbugani, mgombea ubunge wa CCM, Stanslaus Mabula,
alimfungia kazi kwa mkutano mkubwa uliofanyika katika Kata ya Mabatini,
ambapo maelfu ya watu walifurika kwenye uwanja wa Kabengwe Hill,
kusikiliza sera za CCM.
Baada ya mkutano huo ulioanza saa
9:00 mchana hadi saa 12:00 jioni, maelfu ya wananchi na wana CCM walijibu
maandamano ya Wenje kwa kuandamana kutoka Kabengwe Hill hadi kwenye ofisi za
CCM, Wilaya ya Nyamagana na kusabaisha barabara kuu ya Mwanza-Musoma isipitike
kirahisi kwa muda wa saa nzima.
Kufuatia hali hiyo, wafuasi wa
CHADEMA waliokuwa wakirudi maeneo waliyotoka, roho ziliwauma kutokana na Wenje
kuwatangazia kuwa Mabula ameahirisha mkutano wake baada ya kuambulia watu 16.
Wafuasi hao waliingilia kuvuruga
maandamano hayo, wakiwatukana, kuzomea na kuwashambulia baadhi ya akina mama
wanachama wa CCM, hali iliyosabisha vurugu za hapa na pale, ambazo
zilidhibitiwa na polisi na kuwatia mbaroni baadhi ya vijana walioanzisha vurugu
hizo.
Wenje akitumia muda mwingi
kuwashambulia Mabula na Katibu wa UVCCM wa Wilaya ya Nyamagana, Hussein Khim.
Vigogo wa CHADEMA waliohudhuria
mkutano huo ili kumsitiri Wenje ni pamoja na wagombea James Lembeli (Kahama),
Suzan Lyimo (Viti Maalum), Ester Bulaya (Bunda), Vicent Nyerere (Musoma Mjini),
Patrobas Katambi (Shinyanga Mjini) na John Heche (Tarime Vijijini).
Wengine pamoja na wagombea wa
majimbo ya Misungwi ni Hamis Mgawo (Sengerema), Kalwinze Ngongoseke (Magu),
Yusuph Kazi, Ester Matiko (Tarime Mjini) na Highness Kiwia (Ilemela).
No comments:
Post a Comment