Sunday 29 October 2017

JPM ATEUA WAKUU WAPYA SITA WA MIKOA


RAIS Dk. John Magufuli, amefanya uteuzi wa wakuu wapya wa mikoa, makatibu wakuu na manaibu katibu wakuu.

Katika uteuzi huo, uliotangazwa kwa vyombo vya habari jana na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, Rais Magufuli amewateua wakuu wapya wa mikoa sita huku akiwapandisha wakuu wa wilaya watatu.

Akitangaza uteuzi huo, Balozi Kijazi aliwataja wakuu wa wilaya waliopanda cheo, mikoa yao ikiwa kwenye mabano kuwa ni Alexander Mnyeti (Manyara), Joackim Wangabi (Rukwa) na Robert Gabriel (Geita).

Kabla ya uteuzi huo, Mnyeti alikuwa mkuu wa wilaya ya Arumeru, Gabriel alikuwa mkuu wa wilaya ya Korogwe wakati Wangabi alikuwa mkuu wa wilaya ya Nanyumbu.

Wakuu wengine wapya walioteuliwa ni Adam Malima, anayekwenda mkoa wa Mara, Christina Mndeme, aliyeteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Dodoma na Gasper Nyakemwa, aliyeteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Mtwara.

Aidha, Rais Magufuli amewateua IGP wa zamani, Ernest Mangu na Katibu Mkuu wa zamani, Azizi Mlima kuwa mabalozi wapya. Vituo vyao watapangiwa baadaye.

Katika uteuzi huo, Rais Magufuli pia amewapandisha manaibu katibu wakuu saba kuwa makatibu kamili wa wizara, amewahamisha makatibu wakuu wanne na naibu katibu mkuu mmoja kwenda wizara nyingine.

Ofisi ya Rais Ikulu, Katibu Mkuu anaendelea kuwa, Alphayo Kidata; Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Katibu Mkuu anakuwa Laurian Ndumbaro na Naibu wake ni Doroth Mwaluko,

TAMISEMI: Katibu Mkuu anaendelea kuwa Injinia Mussa Iyombe, akisaidiwa na Zainabu Chande (Afya) na Dickson Nzunda (Elimu).

Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira: Katibu Mkuu ni Injinia Joseph Malongo, naibu wake ni Butamo Phillipo.

Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu: Katibu Mkuu ni Erick Shitindi, akisaidiwa na manaibu Maimuna Tarishi na Faustine Kamuzora.

Wizara ya Kilimo: Katibu Mkuu ni Mathew Ntigumwa akisaidiwa na Dk. Thomas Kashillilah.

Wizara ya Mifugo na Uvuvi: Katibu Mkuu ni Maria Mashingo (Mifugo) na Yohana Budeba (Uvuvi).

Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano: Katibu Mkuu ni Leonard Chamuliko, Injinia Joseph Nyamuhega, Maria Sasabwe na Anjelina Madete.

Wizara ya Fedha: Katibu Mkuu ni Dotto Mgisha, akisaidiwa na Susan Mkapa, Amina Shabani na Dk. Khatib Kazungu.

Wizara ya Nishati: Katibu Mkuu ni Khamisi Mwinyimvua

Wizara ya Madini: Katibu Mkuu ni Simon Mpanjira.

Wizara ya Katiba na Sheria: Katibu Mkuu ni Sifuni Mchome, akisaidiwa na Amon Mpanju.

Wizara ya Ulinzi: Katibu Mkuu ni Dk. Florence Turuka, akisaidiwa na Immaculata Ngwala.

Wizara ya Mambo ya Ndani: Katibu Mkuu ni Meja Jenerali Projes Rwegasira, akisaidiwa na Balozi Hassan Simbayahaya.

Wizara ya Maliasili na Utalii: Katibu Mkuu ni Meja Jenerali Gaudence Milanzi, akisaidiwa na Dk. Aloyce Nzuki.

Wizara ya Ardhi: Katibu Mkuu ni Doroth Mwanyika, akisaidiwa na Dl. Moses Kasiluka.

Wizara ya Viwanda na Biashara: Katibu Mkuu ni Profesa Elisante Ole Gabriel, akisaidiwa na Ludovick Mhiye na Profesa Joseph Mushashwaya.

Wizara ya Elimu: Katibu Mkuu ni Leonard Akwilapo, akisaidiwa na Profesa Hapifan Mdoe na Avemaria Semakafu.

Wizara ya Afya: Katibu Mkuu ni Mpoki Olusibisya, akisaidiwa na Sihaba Mkinga.

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo: Katibu Mkuu ni Susan Mlawi, akisaidiwa na Nicholaus William.

Wizara ya Maji: Katibu Mkuu ni Dk. Kitilya Mkumbo, akisaidiwa na Injinia Emmanuel Kalobelo.

Wizara ya Mambo ya Nje: Katibu Mkuu anakuwa Dk. Adolph Nkenda, akisaidiwa na Balozi Ramadhani Mwinyi.

Kwa mujibu wa Balozi Kijazi, wateule hao wapya wanatarajiwa kuapishwa leo, katika hafla itakayofanyika Ikulu, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment