Monday 13 February 2017

RC MAKONDA AKABIDHI ORODHA YA MAJINA 97 YA WAUZA DAWA YA KULEVYA KWA KAMISHNA MKUU WA MAMLAKA YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA JIJINI DAR LEO


Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akionyesha majina mengine 97 ya wauza Dawa za Kulevya awamu ya tatu kwa Bw. Rogers William Sianga kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya ili yaanze kushughulikiwa.RC Makonda amesema awamu hii itaitikisa nchi kwani wameanzia toka awamu ya tatu iliyoongozwa na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, ya nne Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na hii ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli, Katika mkutano uliofanyika kwenye ukubi wa Mwalimu Nyerere JNCC.


Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akikabidhi majina mengine 97 kwa kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa Bw. Rogers William Sianga, kuwa ili yaanze kushughulikiwa.Rc Makond amesema awamu hii itaitikisa nchi kwani wameanzia toka awamu ya tatu iliyoongozwa na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, ya nne Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete na hii ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akizungumza katika mkutano huo,ambapo amekabidhi majina mengine 97 ya awamu ya tatu kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya,Bw. Rogers William sianga ili yaanze kushughulikiwa.


Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akizungumza jambo na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Rogers William Sianga katika mkutano maalum wa kutoa tathmini ya kampeni ya kutokomeza biashara haramu ya madawa ya kulevya katika mkoa wa Dar es salaam na nchi nzima kwa ujumla.


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Kamishna Saimon Sirro akizungumza wakati akitoa taarifa ya kampeni hiyo leo.

No comments:

Post a Comment