Thursday 21 September 2017

ASKARI WA JWTZ AUAWA DRC



JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limesema askari wake, Praiveti Mussa Jumanne, ambaye alikuwa katika ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), amefariki.
Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano ya jeshi hilo kwa vyombo vya habari jana, ilisema kuwa askari huyo alifariki baada ya kushambuliwa kwa kupigwa risasi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, askari huyo alipigwa risasi na kundi la waasi nchini humo, katika tukio lililotokea Septemba 17, mwaka huu.
Kufuatia shambulizi hilo, taarifa hiyo ilisema Umoja wa Mataifa (UN), umeunda Bodi ya Uchunguzi kwa ajili ya kuchunguza tukio hilo.
Aidha, maofisa na askari wa JWTZ, wanaendelea  na majukumu yao katika operesheni hiyo DRC.
Imeongeza kuwa, Umoja wa Mataifa unaandaa utaratibu wa kuuleta nchini mwili wa marehemu, ambapo taratibu za mapokezi, kuaga mwili na mazishi zitatolewa baadaye.

No comments:

Post a Comment