TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetangaza
uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 43, utakaofanyika Novemba 26, mwaka huu.
Taarifa iliyotolewa jana, kwa vyombo vya habari na
Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage, ilisema uchaguzi huo unafanyika
kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo baadhi ya madiwani kufariki dunia.
Alizitaja sababu zingine kuwa ni baadhi ya madiwani
kujiuzulu, kutohudhuria vikao na wengine ushindi wao kutenguliwa na mahakama.
Mwenyekiti huyo
alizitaja kata hizo na mikoa kuwa ni Arusha (Musa, Muriet, Ambureni, Ngabobo,
Maroroni, Leguruki, Makiba na Moita), Dar es Salaam (Mbweni, Kijichi na
Saranga).
Zingine ni Dodoma
(Chipogolo), Geita (Bukwimba na Senga), Iringa ( Kitwiru na Kimala),
Kilimanjaro (Bomambuzi, Mnadani, Machame Magharibi na Weruweru), Lindi (Chikonji na Mnacho).
Kata zingine ni
Manyara ( Nangwa), Mbeya (Ibighi),
Morogoro (Kiloka na Sofi), Mtwara
( Milongodi, Reli na Chaninguo), Mwanza
( Kijima na Mhandu), Rukwa (
Sumbawanga), Ruvuma (Lukumbule,
Kalulu na Muongozi) na Singida (Siuyu).
Zingine
ni Simiyu (Nyabubinza), Songwe ( Dalambo),
Tabora ( Nata na Muungano) na
Tanga ( Majengo, Lukuza na Mamba).
Jaji
Kaijage alisema, wameamua
kutangaza uwepo wa uchaguzi huo, baada
ya waziri mwenye dhamana ya
serikali za mitaa kuwataarifu uwepo wa nafasi wazi za madiwani
katika kata hizo zilizoko katika
halmashauri 36, kwenye mikoa 19
ya Tanzania Bara.
Alibainisha kuwa kifungu cha 13 (1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, kinampa mamlaka waziri
mwenye dhamana ya serikali za mitaa,
kutoa taarifa kuhusu kuwepo kwa nafasi
wazi za madiwani katika kata husika.
Jaji Kaijage alisema baada
ya kupokea taarifa hiyo na kwa
kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(3) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, wana wajibu wa kuitisha na kuendesha uchaguzi mdogo katika kata hizo.
Alisema
ratiba ya mchakato
wa uchaguzi huo
inatarajia kuanza Oktoba 26, mwaka huu, ambapo kutafanyika uteuzi wa wagombea udiwani na kampeni zitaanza
Oktoba 27 na kumalizika Novemba 25,
mwaka.
Jaji Kaijage alitoa wito kwa vyama vya siasa na
wadau wote wa
uchaguzi, kuzingatia matakwa ya
Katiba, Sheria ya
Uchaguzi ya Serikali
za Mitaa, Kanuni
za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Madiwani) za mwaka 2015.
Pia, maadili ya uchaguzi wa Rais, wabunge na
madiwani ya mwaka 2015, pamoja na maelekezo yote yaliyotolewa au yatakayotolewa
na NEC wakati wa
uchaguzi huo.
No comments:
Post a Comment